Random Post

Tuesday, March 15, 2016

games

NJIA ZA KUMWANDAA MTOTO KUWA NA UPEO MKUBWA(AKILI)

Watoto ni wepesi kushika vitu na ni waelewe sana ,wanakuwa kulingana na malezi wanayopewa na wazazi. Wazazi wengi wanaamini mtoto huanza kufunzwa akiwa miaka 3-4 hapana tunakosea sana wenzetu nchi zilizo endelea wanaanza funza watoto wakiwa na miezi 6 hufunzwa kila vitu kulingana na umri mfano kusomewa vitabu mzazi unaweza ukaona haelewi hapana kichwa kinazoea kile anachofunzwa mara kwa mara  .


Ukimwandalia mtoto msingi mzuri  tangu udogoni basi ana nafasi nzuri ya kuwa na upeo(akili) na  uwelewa mkubwa.Wazazi wengi wanaachia watoto wakiamini kila kitu watafunzwa shule ,hapana ni makosa mzazi inakubidi uchukue nafasi yako  pia  kuhakikisha unampa mwongozo bora mtoto .
Watoto wengine ni wazito kuelewa ️au kushika vitu kwa haraka hivyo vizuri akanza kufunzwa mapema.Maandalizi mazuri kwa mtoto yatamjenga kiakili na kumfanya kuwa bright. Hakuna mtoto mjinga duniani ni wazazi tu kukosea kuto kuwapa misingi bora watoto tangu wakiwa na umri mdogo.


ujue ratiba yake akitoka shule anatakiwa kufanya nini,atacheza na wenzake kupumzisha kichwa kumbuka michezo ni muhimu kiafya,baada ya michezo afanye kazi za shule kwa kumsaidia,muulize leo shule wamefanya nini ?kipi kilimfurahisha? nini kilimkasirisha? ,masomo yalikuwaje itakusaidia kujua maendeleo yake ya shule na mahusiano yake na walimu na wanafunzi wenzake ,na unaweza mwelekeza homework yake

Wale wadogo wasio enda shule miezi 9-mpaka miaka 3 nao vile vile anatakiwa tengewa mda Wake ,anavyozidi kukua anazoea ile ratiba na kukaa kichwani kwamba nitacheza ila kunamda nitakaa kusoma hata kama dakika 10-20

Related Posts:

  • FAIDA ZA MATIKITI MAJI FAIDA ZA TIKITI MAJI. Tikiti maji ni tunda ambalo kisayansi hujulikana kama Citrullus lanatus katika familia yaCucurbitaceae, a… Read More
  • MAGONJWA YA NGOZI Mapunye na athari kwa ngozi yako Ni matumaini yangu kuwa hamjambo wapenzi wasomaji wa blog yetu ya watoto karibuni katika makala nyengine ya Ijue Af… Read More
  • TUPANDE MITI YA MATUNDA TUPANDE MITI YA MATUNDA KUKIDHI KIWANGO KINACHOHITAJIKA KWA SIKU. Kila hatua utakayochukua ya kula zaidi matunda na mboga mboga, itakusaidia w… Read More
  • ATHARI ZA SPIKA ZA MASIKIONI SPIKA ZA MASIKIONI ZAWEZA KUSABABISHA UZIWI. Sauti kutokana na matumizi mabaya ya spika za masikioni (earphones & headphones) zaweza kutu… Read More
  • games NJIA ZA KUMWANDAA MTOTO KUWA NA UPEO MKUBWA(AKILI) Watoto ni wepesi kushika vitu na ni waelewe sana ,wanakuwa kulingana na malezi wanayopewa n… Read More

0 comments:

Post a Comment